

Kwa zaidi ya miaka mitano, Mradi wa Usalama wa Umiliki wa Ardhi kwa Wanawake (WOLTS) umekuwa ukichunguza uhusiano wa kijinsia na ardhi katika jamii za wafugaji zilizoathiriwa na uchimbaji wa madini Mongolia na Tanzania. Lengo limekuwa ni kutengeneza mbinu ya ushiriki wa jamii kwa muda mrefu na kujenga uwezo wa kulinda na kusaidia haki za ardhi za watu wote walio katika mazingira magumu na hivyo kuelekeza nguvu katika usawa wa kijinsia, usimamizi na umiliki wa ardhi kwa mfumo ambao utarahisisha maboresho katika haki za ardhi kwa jamii yote.
Mradi umeonyesha kuwa kuwekeza katika kundi la wasaidizi wa jinsia na ardhi, wanawake na wanaume, inaweza kuleta mabadiliko makubwa kwa wanawake na jamii kwa ujumla.. Wasaidizi hao waliopata mafunzo kupitia mradi wa WOLTS wanaimarisha mifumo ya utawala kwenye ngazi ya jamii ili kuimarisha na kulinda haki za wanawake na makundi mengine yaliyo katika mazingira magumu na kuboresha haki za ardhi kwa wanawake na jamii. Hadi sasa, ushahidi unaonyesha kuwa mbinu ya WOLTS (kuwekeza katika wasiadizi wa jinsia na ardhi) inaweza kusaidia kuiwezesha jamii kupambana na kanuni za mifumo dume na kuleta mabadilko katika unyakuzi wa ardhi kwa nchi zinazoendelea. Katika jamii za majaribio, mbinu ya WOLTS ilifichua fursa za uongozi kwa wanawake, mabadiliko ya kanuni za kijamii ndani ya kaya, na kuongeza ufahamu wa unyanyasaji wa kijinsia.
Katika mkutano huo kwa njia ya wavuti, kiongozi wa timu ya WOLTS, Elizabeth Daley, alitoa muhtasari wa mradi huo, matokeo yake na uwezekano wa kutumiwa katika maeneo mengine. Michael Taylor, Mkurugenzi wa International Land Coalition, alizungumzia mtazamo wa ulimwengu juu ya uwezekano wa mradi kuchangia utawala bora wa ardhi kwa mabilioni ya watu wanaotegemea haki za ardhi zajamii. Washiriki waandamizi wa timu ya WOLTS, Joyce Ndakaru (HakiMadini, Tanzania) na Narangerel Yansanjav (People Centered Conservation, Mongolia) walitoa mifano kutoka nchi zao juu ya matokeo chanya ya kufundisha wasaidizi wa jamii juu ya masula ya jinsia na ardhi, na matumizi mapana ya matokeo ya mradi huo hadi sasa.
Mwenyekiti:
Christopher Tanner, Mokoro
Wawasilishaji:
Elizabeth Daley, Mokoro
Michael Taylor, International Land Coalition
Joyce Ndakaru, HakiMadini
Narangerel Yansanjav, People Centered Conservation
Rekodi ya mkutano kwa njia ya wavuti inapatikana hapa:
Auteurs et éditeurs
The vision of the Land Portal Foundation is to improve land governance to benefit those with the most insecure land rights and the greatest vulnerability to landlessness through information and knowledge sharing.
We are an international development consultancy working to improve the wellbeing and opportunities of poor and vulnerable people, by supporting sustainable economic and social development.
The International Land Coalition (ILC) is a coalition of civil society and intergovernmental organizations promoting secure and equitable access to and control over land for poor women and men thro
HakiMadini is rights based not for profit organization with a mission to advance the rights of marginalized Tanzanians through research, education and development projects
HakiMadini essentially started as a reaction to the human rights abuses that were occurring during late 1990s in mining communities.
Our Core Values
- Integrity
- Team work & Volunteerism
- Transparency & Accountability
- Networking & Collaboration
Vision
To become an organization that shaped Mongolia in a positive way.
Mission
PCC is a Mongolian NGO established in 2006, which aims to promote the protection of natural resources through support to the activities of local residents and civil society, with a strong commitment to addressing issues for gender equality and vulnerable groups.
Values